MTOTO AFARIKI DUNIA BAADA YA KUPIGWA NA BABA YAKE MZAZI MKOANI RUKWA.


Mtoto mwenye umri wa miaka 13   mkazi  wa kijiji cha santamalia  kata ya Matai  wilayani Kalambo mkoani Rukwa  Benedkti Salum  amefariki  dunia    kupigwa    kwa  ngumi  na  mateke  na baba yake mzazi  kutokana na  ulevi wa  kupindukia.
Wakiongea  kwa  masiko  makubwa   huku  wakilia  kwa  uchungu  mkubwa  ndugu   wa mtoto  huyo akiwemo   mama  mzazi  wa mtoto huyo  Hilda Mpangamila , wamsema  tukio   hilo  limetokea  baada  ya  baba   wa     mtoto huyo     kumvamia  mtoto  wake  nyakati  za usiku wakati  akiwa amelewa    kwa  kumpiga  na ngumi na  mateke  na  kupelekea   kufariki  dunia.

wamesema  kufuatia  kipigo  hicho    waliamua  kumkimbiza  kwenye kituo  cha  afya  matai ambako  aliweza  kufariki dunia  na  kuwa   licha   ya  mtoto  wake  kupigwa   lakini  hata  yeye  kama mama mzazi  alipigwa  vikari  na  kuwa  tukio  hilo lilitokea  wakati  mumewe  akiwa  amelewa vibaya.

Rafael  Sinyangwe  ambae ni  mwenyekiti  wa  kijiji   hicho, amebainisha  kuwa   hilo  ni  tukio   la   tatu  kwa   mtuhumiwa  huyo  kwani  amekuwa  akiwapiga  ndgu zake   kila  wakati  na  kufikia   hatua   nya  kufanya  mauaji  dhidi   ya  mtoto  wake.

Diwani wa kata hiyo Lejiusi Boimanda  amemtaja  mtuhumiwa  kuwa  ni  pyusi Salimu   na  kulani   vikali kitendo hicho na kuishauri jamii kuacha  tabia  ya   kujichukulia   sheria mkoanoni.

Katibu tarafa   ya  matai  Endru Manyema Ngindo , amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema  jeshi  la  polis  wilayani  humo  lilifika  eneo  la  tukio  na  mtuhumiwa  ambae ni baba  mzazi  wa marehemu  amekamatwa .

Written By Peter kapola.
Share on Google Plus

About KAPOLA NEWZ TV..✍️

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment