DK MWAKYEMBE AWAAMBIA WADAU WA MICHEZO CHA KUFANYA ILI MAMBO YAENDA VIZURI

mwakyembe 

Waziri mpya wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amewataka wanamichezo kumpa ushirikiano katika kuendeleza gurudumu la maendeleo.

Dk Mwakyembe ambaye amechukua nafasi ya Nape Nnauye amesema anaweza kufanya vizuri kama watashirikiana pamoja na wadau wa michezo.

“Tukishirikiana kila jambo litaenda vizuri, serikali inataka mabadiliko, inataka mafanikio na hii ni kwa faida ya wanamichezo. Tushirikiane,” alisema.
 
Jana, Dk Mwakyembe alikaa kikao cha kwanza cha Kamati ya Serengeti Boys na baadaye akaenda Uwanja wa Taifa kuiunga mkono Taifa Stars iliyokuwa inacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Botswana na kuibuka na ushindi wa mabao 2-0, yote yakifungwa na nahodha Mbwana Samatta.

Share on Google Plus

About KAPOLA NEWZ TV..✍️

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment